Friday, December 27, 2013

RAMSEY KUSUGUA BENCHI MPAKA MWAKANI KUTOKANA NA MAJERUHI.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amebainisha kuwa kiungo wake mahiri Aaron Ramsey atakosa mechi zote za kipindi hiki cha sikukuu baada ya kupata majeruhi katika mchezo walioshinda kwa mabao 3-1 dhidi ya West Ham United jana. Nyota huyo wa kimataifa wa Wales atakosa mchezo wa ugenini dhidi ya Newcastle United Jumapili na pia mchezo mwingine utakaochezwa katika Uwanja wa Emirates dhidi ya Cardiff City mwaka mpya. Wenger aliwaambia waandishi wa habari kuwa Ramsey ameumia msuli wa paja na hajui ni kipindi gani atakaa nje ila anafahamu hataweza kucheza tena katika kipindi cha sikukuu kilichobakia. Kocha huyo pia alikisifu kikosi chake kwa mchezo mzuri ambao uliwawezesha kutoka nyuma na kushinda mchezo huo muhimu na kuwafanya kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment