Friday, December 27, 2013

MOYES ATAMBA UNITED KUTETEA TAJI LAKE.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, David Moyes ametamba kuwa kikosi chake kinaweza kutetea taji lao la Ligi Kuu nchini Uingereza baada ya kushinda mchezo wao dhidi ya Hull City kwa mabao 3-1. United walijikuta wakiwa nyuma kwa mabao 2-0 ndani ya dakika 15 za kwanza mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa KC lakini walipambana na kuhakikisha wanasawazisha na baadae kuongeza lingine na kuondoka na alama zote tatu. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Moyes amesema kuwa nyuma na baadae kupata matokeo ya ushindi ni jambo hakulitegemea lakini wachezaji wake wameshawahi kufanya hivyo huko nyuma. Moyes amesema watajitahidi kadri ya uwezo wao kujaribu kupunguza pengo la alama katika msimamo wa ligi kwasababu anaamini bado wana nafasi ya kutetea taji lao.

No comments:

Post a Comment