Friday, December 27, 2013

UTEAUZI WANGU NI KAMA KAMARI - SHERWOOD.

TIM Sherwood amekiri kuwa uteuzi wake kama kocha mkuu wa Tottenham Hotspurs ni uamuzi wa hatari uliochukuliwa na mwenyekiti Daniel Levy. Akizungumza mara baada ya timu hiyo kutoka sare ya bao 1-1 na West Bromwich ukiwa ni mchezo wake wa kwanza toka apate kibarua hicho, Sherwood amesema uteuzi wake ni kama kamari kwasababu hajawahi kufanya kazi kama kocha mkuu. Pamoja na hayo lakini Sherwood anaamini kuwa anaweza kupata mafanikio kwasababu wako wengi walioanza kama yeye na baadae kufanikiwa. Sherwood alipewa kibarua hicho Jumatatu akichukua nafasi ya Andres Villas-Boas aliyetimuliwa wiki iliyopita.

No comments:

Post a Comment