Friday, December 27, 2013

BOATENG ASHAMBULIWA MTAANI HUKO UJERUMANI.

POLISI nchini Ujerumani wanachunguza madai ya kushambuliwa kwa kiungo wa kimataifa wa Ghana Kevin-Prince Boateng siku ya Christmass baada ya mabishano humo Kaarst. Polisi wa mji wa Dusseldorf wamethibitishia wana habari kuwa mtu huyo mwenye umri wa miaka 26 aliyehusika katika tukio hilo ni Boateng ambaye anacheza katika klabu ya Schalke 04. Taarifa hiyo ya polisi ilidai kuwa Boateng ambaye ni mkazi wa Meerbusch alishambuliwa na mtu asiyejulikana wakati akikatiza mtaani. Nyota huyo ambaye anaripotiwa kuumia kidogo, alirejea nyumbani baada ya tukio hilo na kisha kupiga simu polisi.

No comments:

Post a Comment