Monday, December 30, 2013

MAN CITY NDIO WENYE NAFASI YA KUNYAKUWA TAJI LA LIGI KUU - MOURINHO.

MENEJA wa klabu ya Chelsea, Jose Mourinho anafikiri kuwa Manchester City bado ndio wenye nafasi ya kunyakuwa taji la Ligi Kuu nchini Uingereza pamoja na ushindi wa timu yake dhidi ya Liverpool. Kikosi cha Mourinho kilifanikiwa kutoka nyuma na kufanikiwa kuibuka na ushindi muhimu wa mabao 2-1 yaliyofungwa na Eden Hazard na Samuel Eto’o huku bao la Liverpool likifungwa na Martin Skrtel. Chelsea sasa wamefanikiwa kupata ushindi wao wan ne mfululizo katika Ligi Kuu huku wakiingia mwaka 2014 wakiwa nyuma kwa alama mbili mbele ya vinara Arsenal lakini Mourinho anaamini kuwa City wanaoshika nafasi ya pili ndio tishio zaidi katika mbio hizo. Mourinho amesema kuna tofauti kubwa kati ya City na timu zingine na sio ubora kwasababu timu zingine zina ubora pia lakini ni ukomavu, nguvu na uzoefu wa wachezaji ndio unawatofautisha na timu zingine.

No comments:

Post a Comment