Monday, December 30, 2013

SCHUMACHER TAABANI BAADA YA KUPATA AJALI AKITELEZA KATIKA BARAFU.

DEREVA nyota wa zamani wa mashindano ya langalanga kutoka Ujerumani, Michael Schumacher yuko katika hali mbaya baada ya kupata ajali wakati akiteleza katika barafu huko Ufaransa. Schumacher mwenye umri wa miaka 44 ambaye ni bingwa wa dunia mara saba wa langalanga alijibamiza kichwa katika jiwe alipoanguka wakati akiteleza ambapo sasa anatumia mashine maalumu akiwa hajitambui baada ya kufanyiwa upasuaji wa ubongo. Meneja wake, Sabine Kehm amesema Schumacher ambaye alikuwa na mwanae wa kiume wakati wa tukio hilo alikuwa amevaa kofia ngumu wakati alipojibamiza kichwa katika jiwe. Schumacher alichukuliwa na helikopta kutoka katika milima ya Ufaransa alipopata ajali hiyo na kuwahishwa katika kituo cha afya cha karibu lakini baadae alihamishwa katika hospitali ya Chuo Kikuu cha Grenoble ambayo ina vifaa vingi na kisasa zaidi.

No comments:

Post a Comment