Monday, December 30, 2013

BOATENG ALAZWA BAADA YA KUSHAMBULIWA CHRISTMAS.

KIUNGO wa klabu ya Schalke 04, Kevin-Prince Boateng amelazwa hospitalini baada ya kushambuliwa siku ya Christmas. Nyota huyo wa kimataifa wa Ghana mwenye umri wa miaka 26 aliumia mbavu, mgongo na shingo wakati wa tukio hilo lililotokea katika mji wa Kaarst ulio karibu na jiji la Dusseldorf. Taarifa ya polisi ilidai kuwa Boateng alishambuliwa na mtu ambaye hakujulikana mara moja wakati akikatiza katika mitaa ya mji huo. Boateng alijiunga na Schalke kutoka AC Milan kwa ada ya euro milioni 12 Agosti mwaka huu.

No comments:

Post a Comment