Monday, December 30, 2013

MOYES AIKUMBUKA KOMBINESHENI YA VAN PERSIE NA ROONEY.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, David Moyes anategemea washambuliaji wake Robin van Persie na Wayne Rooney kuwa fiti mwaka mpya baada ya nyota huyo wa kimataifa wa Uholanzi kuanza mazoezi mepesi. Van Persie amekuwa akisumbuliwa na majeraha ya paja, kidole gumba na kiuno msimu huu na majeraha yake ya hivi karibuni aliyapata wakati akipiga mpira wa kona katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa barani Ulaya dhidi ya Shakhtar Donetski. Moyes ambaye ameshuhudia kikosi chake kikipata ushindi wa sita mfululizo katika mashindano yote amesema Van Persie tayari ameanza mazoezi mepesi hivyo anaweza kurejea uwanjani hivi karibuni. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa siku nyingi hawajashuhudia Van Parsie na Rooney wakicheza pamoja hivyo itakuwa vyema wakikutana tena ili kuongeza nguvu katika safu yake ya ushambuliaji.

No comments:

Post a Comment