Monday, December 30, 2013

WILLIAMS NDIO ANAYENIFANYA NI BORA - AZARENKA.

MWANADADA nyota katika tenisi Victoria Azarenka wa Belarus anafikiri hasimu wake Serena Williams wa Marekani ndio anamfanya awe mchezaji bora ambapo wanatarajia kukutana tena katika michuano ya kimataifa ya Brisbane na baadae michuano ya wazi ya Australia. Azarenka anayeshika nafasi ya pili katika orodha za ubora duniani atakutana na Williams anayeshika nafasi ya kwanza kama wachezaji hao wakifanikiwa kufika fainali ya michuano hiyo inayotarajiwa kuchezwa mwishoni mwa wiki ijayo katika uwanja wa Pat Rafter jijini Abu Dhabi. Akihojiwa Azarenka mwenye umri wa miaka 24 amesema ni jambo jema kuwa na hasimu kama Williams kwasababu inamjenga kama mchezaji kutokana na mazoezi ya nguvu anayofanya ili aweze kumudu kupambana na yoyote. Azarenka na Williams wamekuwa mahasimu kwa muda lakini ni Williams ndio mwenye rekodi nzuri zaidi baada ya kushinda mechi 13 dhidi ya tatu za Azarenka walizokutana.

No comments:

Post a Comment