Tuesday, December 31, 2013

BAYERN INAWEZA KUTAWALA SOKA LA ULAYA KWA MIAKA 10 ZAIDI - HEYNCKES.

MENEJA wa zamani wa klabu ya Bayern Munich ya Ujerumani Jupp Heynckes amedai kuwa timu hiyo inaweza kutawala soka barani Ulaya kwa miaka 10 mingine. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 68 ambaye aliiongoza Bayern kushinda mataji msimu uliopita amesema kikosi hicho ambacho hivi sasa kinanolewa na Pep Guardiola kinaweza kuendelea kutawala soka la Ulaya kwa muongo mmoja zaidi. Heynckes amesema kwa jinsi kikosi hicho kilivyokuwa na wachezaji chipukizi hakuna shaka kwamba wataendelea kutamba kwa kipindi kirefu huko mbele. Kocha huyo alichagua kustaafu kufundisha soka baada ya kuinoa Bayern pamoja na kupata ofa kutoka timu mbalimbali barani Ulaya.

No comments:

Post a Comment