Tuesday, December 31, 2013

RAIS WA IOC AMTUMIA SALAMU ZA RAMBIRAMBI RAIS PUTIN.

RAIS wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki-IOC, Thomas Bach amesema ana uhakika kuwa Urusi itaandaa michuano ya olimpiki ya majira ya baridi jijini Sochi iliyokuwa salama. Bach alimtumia salamu za rambirambi Rais Vladimir Putin kufuatia mashambulio ya mabomu ya kujitoa muhanga katika treni na basi matukio ambayo yamepelekea vifo vya watu 31. Matukio hayo yametokea ukiwa umebaki mwezi mmoja pekee kabla ya kuanza michuano hiyo. Bach amesema matukio hayo hayakubaliki na hayawezi kurudisha nyuma dhamira ya nchi hiyo kuwa mwenyeji wa michuano hiyo ambapo kwa pamoja wanaweza kumshinda adui.

No comments:

Post a Comment