Tuesday, December 31, 2013

MPUTU AACHWA KIKOSI CHA CHAN.

KOCHA wa timu ya taifa ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo-DRC, Mutumbile Santos ametaja kikosi chake kitakachoshiriki michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani mwakani huku akimuacha Tresor Mputu ambaye amejiunga na klabu ya Kabuscorp ya Angola akitokea TP Mazembe. Hakuna sababu yoyote iliyotolewa ya kuachwa kwa mshambuliaji huyo ingawa hata hivyo amekuwa akitishia kutojumuika na kikosi hicho kama baadhi ya mambo ya kimaslahi hayatarekebishwa. Mputu ndio aliteuliwa kuwa mchezaji bora wa mashindano hayo mwaka 2009 ambapo nchi yake ilinyakuw ataji hilo. Ni wachezaji wawili pekee waliokuwepo katika kikosi cha mwaka 2009 ndio watashiriki michuano hiyo itakayofanyika Januari nchini Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment