Tuesday, December 31, 2013

HALI YA SCHUMACHER BADO TETE.

FAMILIA ya dereva nguli wa mashindano ya langalanga, Michael Schumacher imeendelea kuwa pembeni ya kitanda cha wakati akipigania maisha yake kufuatia ajali aliyopata wakati akiteleza katika barafu katika milima ya Ufaransa. Meneja wa dereva huyo Sabine Kehm amesema mke Corinna, binti yake Gina Maria na kijana wake wa kiume Mick bado wameendelea kubakia katika hospitali ya Grenoble ili kujua hatma ya mpendwa wao. Schumacher ambaye ambaye ni bingwa wa dunia mara saba wa mashindano ya langalanga alipata majeraha ya kichwani wakati alipoanguka kwenye tukio hilo. Mkuu wa hospitali hiyo profesa Jean-Francois Payen amesema nyota huyo bado ameendelea kubakia katika wodi ya watu wanaohitaji uangalizi maalumu huku akiwa amepewa dozi nzito za usingizi ili ubongo wake uweze kujitibu taratibu baada ya upasuaji.

No comments:

Post a Comment