Tuesday, December 31, 2013

MESSI AHOFIA MAJERUHI.

MSHAMBULIAJI nyota wa Barcelona, Lionel Messi amesema kuwa mwaka ujao anategemea kuepuka majeruhi tofauti ilivyokuwa kwa mwaka huu. Mwaka huu umekuwa sio mzuri kwa Messi baada ya kusumbuliwa na mejeruhi ya mara kwa mara huku akiwa amekaa nje toka mwezi Novemba kwa majeraha ya msuli. Barcelona imekuwa ikihaha kutokana na kumkoa nyota huyo kwa kufungwa na Ajax Amsterdam katika Ligi ya Mabingwa barani Ulaya na Athletic Bilbao katika La Liga lakini sasa inaweza kupumua baada ya Messi kutegemewa kurudi baada ya mapumziko ya majira ya baridi. Akihojiwa na mtandao wa timu hiyo, Messi amesema baada ya kusheherekea sikukuu za mwisho wa mwaka na familia yake atasafiri kuelekea jijini Barcelona kwa ajili ya maandalizi ya mwisho kabla ya kurejea uwanjani.

No comments:

Post a Comment