Tuesday, December 31, 2013

WENGER MAJERUHI WAMUWEKA KATIKA HALI NGUMU.

KLABU ya Arsenal inakabiliwa na balaa la majeruhi wakati wakielekea katika mchezo wao wa mwaka mpya dhidi ya Cardiff City baada ya wachezaji wanne kuondolewa katika orodha ya kikosi kitakachoanza katika mchezo huo. Meneja wa klabu hiyo Arsene Wenger amethibitisha kuwa Olivier Giroud, Aaron Ramsey, Mesut Ozil na Kieran Gibbs hawatakuwepo katika mchezo huo wakati Theo Walcott, Tomas Rosicky, Thomas Vermaelen na Jack Wilshere nao wakiwa katika hati hati ya kucheza. Kwa upande mwingine Wenger amethibitisha kuwa wanatafuta mchezaji muhimu katika kipindi cha usajili wa dirisha dogo huku safu ya ushambuliaji ikipewa nafasi kubwa. Giroud ambaye amekuwa mshambuliaji tegemeo katika kipindi kirefu msimu huu alikaririwa karibuni akidai kuwa klabu hiyo haitaji mshambuliaji mwingine pamoja na yeye kushindwa kufunga mabao mengi.

No comments:

Post a Comment