Wednesday, January 22, 2014

AUSTRALIA OPEN 2014: BINGWA MTETEZI AZARENKA OUT.

BINGWA mtetezi wa michuano ya wazi ya Australia, mwanadada Victoria Azarenka ameng’olewa katika michuano hiyo baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Agnieszka Radwanska katika mchezo wa robo fainali. Katika mchezo huo Azarenka anayeshika nafasi ya pili katika orodha za ubora wa mchezo huo kwa upande wa wanawake alishindwa kutamba mbele ya Radwanska anayeshika nafasi ya tano kwa kufungwa seti 2-1 zenye alama za 6-1 5-7 6-0. Kipigo hicho kinamaliza ubabe wa Azarenka kushinda mechi 18 katika viwanja vya jiji la Melbourne kuanzia mwaka 2012 na kumaanisha kuondolewa kwa nyota wote wanaoshika nafasi ya tatu za juu baada ya Serena Williams na Maria Sharapova kuondolewa mapema. Radwanska sasa atakwaana na Dominika Cibulkova katika mchezo wa nusu fainali baada ya mwanadada huyo kumuondosha Simona Halep katika mchezo war obo fainali.

No comments:

Post a Comment