Wednesday, January 22, 2014

BINGWA CHAN KUNYAKUWA KITITA CHA DOLA 746,463.

PAMOJA na kuenguliwa katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani,CHAN katika hatua ya makundi, timu ya taifa ya Afrika Kusini maarufu kama Bafana Bafana haikutoka mikono mitupu baada ya kukabidhiwa kitita cha dola 175,000 kwa kumaliza katika nafasi ya tatu kwenye kundi lao. Kamati ya Maandalizi ya michuano hiyo imedai kuwa jumla ya fedha zote za zawadi inafikia kiasi cha dola milioni tatu. Bingwa wa michuano hiyo atanyakuwa kitita cha dola 746,463 na mshindi wa pili atachukua kiasi cha 396,270 huku wa tatu na wanne wote wakichukua dola 248,821 kila mmoja. Timu ambazo zitakwamia katika hatua ya robo fainali zitachukua 175,096 huku zile ambazo zimeshika mkia katika kwenye makundi yao zikiambulia dola 92,156 kila moja. Michuano hiyo inayoendelea nchini Afrika Kusini inatarajiwa kufikia tamati yake Februari mosi mwaka huu.

No comments:

Post a Comment