Wednesday, January 22, 2014

MIDO ATEULIWA KUINOA ZAMALEK.

MSHAMBULIAJI wa zamani wa AS Roma ya Italia na Ajax Amsterdam ya Uholanzi, Mido ameteuliwa kuwa kocha mpya wa klabu yake ya nyumbani ya Zamalek. Mido anachukua mikoba ya kocha Helmi Toulan ambaye alitimuliwa kufuatia sare ya bao 1-1 iliyopata Zamalek dhidi ya Haras El-Hodood katika mchezo wa Ligi Kuu nchini Misri. Hiyo inakuwa mechi ya nne kwa Zamalek msimu huu ambapo klabu hiyo inashika nafasi ya nne baada ya kushinda mechi mbili kutoa sare moja na kufungwa moja. Mido ambaye anafikisha umri wa miaka 31 Februari mwaka huu anakuwa kocha mdogo zaidi katika historia ya soka nchini hiyo na hana uzoefu wa kutosha wa kufundisha. Nyota huyo ambaye alianza kusakata kabumbu Zamalek mwaka 1999 kabla ya kwenda kucheza Ulaya ameifungia timu ya taifa ya nchi hiyo mabao 19 katika mechi 51 alizocheza.

No comments:

Post a Comment