Wednesday, January 22, 2014

MAN UNITED MBIONI KUMSAJILI JUAN MATA.

KLABU ya Manchester United ina uhakika wa kumnyakua kiungo Juan Mata kutoka Chelsea kwa ada ya paundi milioni 37 mwishoni mwa wiki hii. Mazungumzo kuhusiana na uhamisho wa kiungo huyo wa kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 25 yamefikia pazuri hivyo kuna uwezekano akafanyiwa vipimo vya afya kabla ya mwishoni mwa wiki. Mata amekuwa akitaka kuondoka Chelsea baada ya kushindwa kumshawishi kocha Jose Mourinho msimu huu. United ambao kwasasa wako katika nafasi ya saba katika msimamo wa Ligi Kuu wako katika changamoto kubwa ya kifedha kama wakishindwa kufuzu michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Ulaya msimu ujao.

No comments:

Post a Comment