Wednesday, January 22, 2014

NEGREDO KUFANYIWA VIPIMO VYA BEGA LAKE.

KLABU ya Manchester City, inatarajiwa kumfanyia vipimo Alvaro Negredo baada ya mshambuliaji huyo kuumia bega lake katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Ligi dhidi ya West Ham United. Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania alianguka vibaya mwishoni baada ya kufunga mabao mawili na kuisadia City kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo huo wa mkondo wa pili. Kocha wa City Manuel Pellegrini alikiri kuwa nyota huyo kuwa katika maumivu makali lakini inabidi wasubiri ili kujua ameumia kiasi gani baada ya kufanyiwa vipimo. Pellegrini pia aliwasifu wachezaji wake kwa kufanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano hiyo kwa kishindo baada ya kuingamiza West Ham kwa jumla ya mabao 9-0 katika mechi za mikondo miwili walizokutana.

No comments:

Post a Comment