Friday, January 24, 2014

AUSTRALIA OPEN 2014 FAINAL: MEN: NADAL VS WAWRINKA, WOMEN: LI NA VS CIBULKOVA

MCHEZAJI nyota wa tenisi anayeshika namba moja katika orodha za ubora kwa upande wa wanaume, Rafael Nadal amefanikiwa kutinga fainali ya michuano ya wazi ya Australia baada ya kumgaragaza Roger Federer wa Switzerland. Nadal ambaye ni raia wa Hispania alifanikiwa kumchakaza mkongwe huyo kwa seti tatu bila majibu zenye alama za 7-6 6-3 6-3 na kutinga hatua hiyo ambapo sasa atakwaana na Stanislav Wawrinka. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 anapewa nafasi kubwa ya kunyakuwa hilo katika fainali itakayochezwa Jumapili hii na kama akifanikiwa atakuwa mchezaji wa tatu kushinda kila taji Grand Slam mara mbili. Mbali na wanaume kwa upande wa wanawake pia kutakuwa na mchezo wa fainali utakaochezwa kesho ambapo mwanadada nyota kutoka China Li Na atachuana vikali na Dominika Cibulkova wa Slovakia. Li Na atakuwa na mategemeo makubwa ya kunyakuwa taji hilo safari hii baada ya kulikosa katika fainali mbili mfululizo zilizopita katika michuano hiyo.

No comments:

Post a Comment