Friday, January 31, 2014

BAADA YA KUMKOSA DRAXLER, WENGER SASA AHAMISHIA NGUVU ZAKE KWA MKONGWE WA SWEDEN KALLSTROM.

MENEJA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amethibitisha kuwa hawezi tena kumsajili kiungo mahiri wa klabu ya Schalke, Julian Draxler baada ya klabu hizo kushindwa kufikia makubaliano. Huku muda wa usajili wa dirisha dogo ukikaribia mwishoni Wenger sasa amehamishia nguvu zake kwa kiungo mkongwe Kim Kallstrom kutoka klabu ya Spartak Moscow ya Urusi ili aweze kuimarisha safu yake ya kiungo ambayo imekumbwa na majeruhi wengi. Arsenal ilishindwa kufikia makubaliano na Schalke baada ya klabu hiyo kutaka kutoa kiasi cha paundi milioni 25 au 30 lakini Wajerumani hao wao walitaka paundi milioni 37.3. Wakati akimkosa Theo Walcott kwa msimu mzima, Aaron Ramsey kwa wiki sita huku Jack Wilshere akiwa katika hatihati ya kucheza katika mechi dhidi ya Cardiff City, Wenger amepania kuongeza nguvu katika kikosi chake ili aweze kuhakikisha wanaweka hai matumaini yao ya kunyakuwa taji la Ligi Kuu.

No comments:

Post a Comment