Friday, January 31, 2014

CHICHARITO KUBAKIA UNITED - WAKALA.

WAKALA wa mshambuliaji nyota wa klabu ya Manchester United, Javier Hernandez maarufu kama Chicharito amedai kuwa mteja wake huyo hawezi kuondoka Old Traford katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo lakini anaweza kuondoka majira ya kiangazi. Nyota huyo wa kimataifa wa Mexico amekuwa akipambana kurejea katika kiwango chake toka awe chini ya David Moyes msimu huu akiwa amefunga mabao mawili katika mechi 14 alizocheza lakini wakala huyo aitwaye Eduardo Hernandez amesema klabu hiyo imesisitiza kuwa bado inamuhitaji nyota huyo. Pamoja na kuwa mkataba wa Chicharito unamalizika majira ya kiangazi mwaka 2015, lakini Hernandez amesema kuna uwezekano mkubwa mteja wake huyo ajaondoka baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu. Wakala huyo aliendelea kudai kumekuwa na vilabu nchini Ujerumani, Ufaransa, Hispania na Italia ambavyo vinahitaji huduma ya nyota huyo hivyo hawezi kujua hali itakavyokuwa baada ya Kombe la Dunia.

No comments:

Post a Comment