Friday, January 31, 2014

KUSHINDA KOMBE LA DUNIA ITAKUWA NGUMU - REUS.

MSHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ujerumani, Marco Reus anaamini kuwa nchi hiyo itakabiliwa na wakati mgumu kushinda taji la Kombe la Dunia mwaka huu lakini akasisitiza kuwa mabingwa hao mara tatu wa michuano hiyo watakwenda Brazil wakiwa na matumaini ya kufika mbali. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 kuna uwezekano mkubwa akawemo katika kikosi cha nchi hiyo kinachonolewa na Joachim Low lakini amekuwa na tahadhari kuhusu uhakika wan chi yake kunyakuwa taji la nne kwenye michuano hiyo. Reus amesema michuano ya Kombe la Dunia ndiyo bora kabisa katika soka hivyo timu zote zonazoshiriki zinakuwa zimejiandaa vyema hivyo lazima hali itakuwa ngumu kwasababu kila timu inataka kushinda taji hilo kama ilivo kwao. Nyota huyo aliendelea kusema kuwa hakuna anayejua kinachoweza kutokea katika mashindano hayo kama vile majeruhi lakini hana shaka kwamba timu yake inaweza kufikia hatua ya fainali.

No comments:

Post a Comment