Friday, January 31, 2014

MKALI WA MIPIRA YA ADHABU, JUNINHO ASTAAFU SOKA RASMI.

BINGWA wa kupiga mipira ya adhabu (free Kick) Mbrazil Juninho Pernambacano ameamua kutundika daruga baada ya kudumu katika ulimwengu wa soka kwa kipindi cha miaka 20. Rais wa klabu ya Vasco da Gama ya Brazil, Roberto Dinamite alikaririwa akidai kuwa amezungumza na nyota huyo na kumhakikishia kuwa ameamua kupumzika rasmi mchezo wa soka. Juninho ambaye amesheherekea siku yake ya kuzaliwa Alhamisi akitimiza miaka 39 ameichezea Vasco da Gama mechi 393 katika vipindi vitatu tofauti. Akiwa na timu hiyo Juninho ameshinda taji la ligi mwaka 1997 na 2000, taji la Klabu Bingwa ya Amerika Kusini mwaka 1998 na Copa Mercosul mwaka 2000 huku akiwa amefunga mabao 76 kwa klabu hiyo yenye maskani yake jijini Rio de Janeiro. Juninho pia amecheza soka kwa mafanikio nchini Ufaransa katika klabu ya Olympique Lyon na kufanikiwa kushinda mataji saba mfululizo ya Ligi Kuu nchini humo kuanzia mwaka 2002 mpaka 2008.

No comments:

Post a Comment