Friday, January 31, 2014

GET WELL SOON FALCAO - RONALDO.

MSHAMBULIAJI wa klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo amemtakia heri ya kupona haraka Radamel Falcao na kudai kuwa soka limhitaji mshambuliaji huyo kwenye Kombe la Dunia. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 anayecheza katika klabu ya Monaco ya Ufaransa, atakuwa nje kwa msimu wote uliobakia baada ya kuchanika msuli wa ndani katika goti lake la kushoto mapema Januari hatua ambayo inaweza kupelekea akaikosa pia michuano ya Kome la Dunia itakayofanyika Juni nchini Brazil. Hata hivyo, madaktari waliomfanyia upasuaji Falcao wamedai kuwa anaweza kupona kwa wakati kwa ajili ya michuano hiyona Ronaldo anamuomba iwe hivyo kwa nyota huyo wa kimataifa wa Colombia. Ronaldo amesema Kombe la Dunia na timu ya taifa ya Colombia wanamsubiri na ana matumaini kuwa atapona haraka na kurejea uwanjani kwa wakati.

No comments:

Post a Comment