Tuesday, January 21, 2014

CHAN 2014: UGANDA YAFUNGISHWA VIRAGO NA MOROCCO.

WAWAKILISHI pekee wa Afrika Mashariki katika michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani,CHAN timu ya taifa ya Uganda wameaga michuano hiyo baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Morocco katika mchezo uliochezwa katika Uwanja wa Cape Town. Uganda walienguliwa kwa kufungwa mabao 3-1 na Morocco katika mchezo mkali wa kundi B ambao kama wangefanikiwa kushinda wangeweza kutinga robo fainali ya michuano hiyo. Katika mchezo mwingine w kundi hilo Burkina Faso nao walifungashwa virago kwa kutandikwa na Zimbabwe kwa bao 1-0. Michuano hiyo inaendelea tena leo ambapo Ethiopia ambao wameshatolewa katika michuano watakamilisha ratiba kwa kuchuana na Ghana katika Uwanja wa Free State, Mangaung huku Congo wakichuana na Libya katika Uwanja wa Peter Mokaba huko Polokwane.

No comments:

Post a Comment