Tuesday, January 21, 2014

BARCELONA KUUKARABATI UWANJA WA CAMP NOU KWA EURO MILIONI 600.

KLABU ya Barcelona imewasilisha mpango wa matengenezo ya Uwanja wa Camp Nou ambao utagharimu kiasi cha euro milioni 600 na kuwa na uwezo wa kuongeza mashabiki kufika 105,000. Mara ya kwanza Barcelona walikuwa wamefikiria kujenga uwanja mpya katika na eneo la Avenida Diagonal ambalo ni kituo kikubwa cha biashara katika jiji hilo lakini mpango huo ulikwama kutokana na gharama kubwa inayokadiriwa kufikia euro bilioni 1.2. Badala yake mabingwa hao watetezi wa La Liga wameamua kutumia nusu ya fedha hizo kuuukarabati uwanjani wa sasa ambapo utahusisha pia ujenzi wa paa kufunika uwanja huo. Rais wa Barcelona, Sandro Rosell amesema umekuwa uamuzi mgumu kutokana na mipango yote miwili kuvutia lakini wameamua kubakia hapo kwasababu ni sehemu ya historia ya klabu hiyo.

No comments:

Post a Comment