Tuesday, January 21, 2014

ANELKA AKABILIWA NA ADHABU KUTOKA FA.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya West Bromwich, Nicolas Anelka atakabiliwa na adhabu ya kufungiwa mechi tano kama akipatikana na hatia na Shirikisho la Soka nchibni Uingereza, FA kwa kuonyesha ishara ya quenelle. Anelka alionyesha ishara hiyo ambayo inadaiwa kutumika salamu ya wafuasi wa Nazi, wakati alipofunga bao dhidi ya West Ham United Desemba 28 mwaka jana. Wadhamini wa West Brom kampuni ya Zoopla wamepanga kukatisha udhamini wao na klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu kutokana na ishara hiyo aliyoonyesha Anelka. Katibu wa mashabiki wa klabu hiyo, Alan Cleverley amesema kama Anelka akikutwa na hatia ya kufanya kitendo hicho cha kibaguzi atakuwa anastahili adhabu yoyote atakayopewa kwasababu vitendo hivyo haviruhusiwi katika soka.

No comments:

Post a Comment