Thursday, January 23, 2014

KAMWAGA AUKWAA UKATIBU SIMBA, ASHA MUHAJI OFISA HABARI MPYA.


KLABU ya Soka ya Simba imefanya mabadiliko ya sekretarieti yake pamoja na kutangaza tarehe ya kufanya Mkutano Mkuu maalumu. Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa klabu hiyo Ismail Aden Rage amesema wamefikia hatua hiyo baada ya kufanyika kwa kikao cha Kamati ya Utendaji. Rage amesema nafasi ya Katibu Mkuu wa klabu sasa itashikiliwa na aliyekuwa ofisa habari wake Ezekiel Kamwaga akisaidiwa na Stanley Philipo, nafasi ya muhasibu ikibakia kwa Eric Sekiete akisaidiwa na Amina Kimwambi. Nafasi ya ofisa habari sasa itashikiliwa na Asha Muhaji huku meneja wa timu akiwa Hussein Mbozi na Issa Mathayo atakuwa msimamizi. Rage pia amesema katika kikao hicho wamepanga Machi 23 mwaka huu kuwa tarehe ya Mkutano Mkuu Maalumu ambao utakuwa na ajenda moja ya kuhusu mabadiliko ya katiba. Wakati huohuo Rage amesema wamepokea barua kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Kamati ya Hadhi za Wachezaji wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA ambayo inawataka klabu ya Etoul du Sahel hadi Januari 27 mwaka huu wawe wametoa maelezo kuhusiana na hela ya mshambuliaji Emmanuel Okwi.

No comments:

Post a Comment