Thursday, January 23, 2014

AUSTRALIA OPEN 2014: LI NA, CIBULKOVA KUKWAANA FAINALI.

MWANADADA nyota katika tenisi kutoka China, Li Na amefanikiwa kutinga hatua ya fainali ya michuano ya wazi ya Australia baada ya kufanikiwa kumchapa chipukizi Euginie Bouchard katika mchezo wa nusu fainali. Li ambaye amepoteza michezo yake yote mitatu ya fainali katika michuano hiyo alifanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kumgaragaza Bourchard wa Canada kwa 6-2 6-4. Mwanadada huyo sasa atakwaana na Dominika Cibulkova wa Canada baada ya nyota huyo kumuondosha Agnieszka Radwanska kwa 6-1 6-2 katika nusu fainali nyingine iliyofabyika katika uwanja wa Rod Laver Arena. Wakati nyota watatu wanashika nafasi za juu katika orodha za ubora duniani kwa upande wa wanawake, Serena Williams, aliyekuwa bingwa mtetezi Victoria Azarenka na maria Sharapova wakiwa wametolewa hiyo itakuwa ni nafasi pekee kwa Li Na kunyakuwa taji hilo katika mchezo wa fainali Ijumaa baada ya kulisotea kwa miaka mitatu mfululizo.


No comments:

Post a Comment