Thursday, January 23, 2014

MAN UNITED YAMNASA MATA.

KLABU ya Chelsea imekubali ofa ya paundi milioni 37 kwa ajili kumuuza kiungo wao nyota wa kimataifa wa Hispania, Juan Mata kwa klabu ya Manchester United. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 25 amefanyiwa vipimo vya afya leo kabla ya kukamilisha uhamisho wake. Mata anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka minne na nusu kuitumikia United. Nyota huyo aliaga wachezaji wenzake na viongozi wa Chelsea katika mazoezi ya timu hiyo huko Cobham jana.

No comments:

Post a Comment