Thursday, January 23, 2014

TULISTAHILI KUCHAPWA NA SUNDERLAND - MOYES.

MENEJA wa klabu ya Manchester United, David Moyes amedai kuwa kikosi chake kilistahili kuenguliwa katika michuano ya Kombe la Ligi na Sunderland jana. Baada ya kushinda mchezo wa nusu fainali ya mkondo wa pili katika Uwanja wa Old Traford timu zililazimika kucheza muda wa nyongeza na baadaye changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kutoka sare kwa mabao 3-3 katika michezo ya mikondo miwili waliyokutana. Katika changamoto ya mikwaju ya penati United walikosa mikwaju minne na kupelekea kutolewa katika michuano hiyo ambapo sasa majirani zao Manchester City watakwaana Sungerland katika mchezo wa fainali utakaochezwa katika Uwanja wa Wembley Machi 12 mwaka huu. Akihojiwa Moyes amesema kikosi chake hakucheza vizuri kustahili kusonga mbele na kuwapongeza Sunderland kuwa walistahili kusonga mbele kutokana na juhudi walizoonyesha.

No comments:

Post a Comment