Friday, January 31, 2014

MADAKTARI WAANZA KUMPUNGUZIA SCHUMACHER DOZI YA USINGIZI ILI AAMKE.

MENEJA wa dereva nyota wa zamani wa mashindano ya langalanga, Michael Schumacher amesema madaktari wanamtibu wameanza kupunguza dozi nzito za usingizi walizompa ili aweze kuamka taratibu. Meneja huyo Sabine Kehm amesema hatua hiyo ni muhimu kwa afya ya Schumacher na inaweza kuchukua muda mrefu. Schumacher alianguka na kuumia kichwani wakati akiteleza katika barafu huko katika milima ya Ufaransa Desemba 29 mwaka jana. Toka kipindi hicho madaktari wamekuwa wamemuweka katika dozi kubwa za usingizi ili ubongo wake uweze kupona wenyewe taratibu kwasababu ya upasuaji mara mbili aliofanyiwa kutokana na ajali aliyopata.

No comments:

Post a Comment