Friday, January 24, 2014

MZUNGUKO WA PILI LIGI KUU KUANZA KUTIMUA VUMBI.

MZUNGUKO wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom-VPL kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza rasmi kesho kwa mechi nne zitakazochezwa katika miji ya Bukoba, Dar es Salaam na Tanga. Mabingwa watetezi Yanga watakuwa wageni wa Ashanti United kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi kutakuwa na mechi kati ya wenyeji Azam FC na Mtibwa Sugar kutoka Morogoro. Coastal Union itaikaribisha Oljoro JKT ya Arusha kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga, huku Kagera Sugar ikiikaribisha Mbeya City kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. Raundi ya 14 ya ligi hiyo itaendelea Jumapili Januari 26 kwa mechi mbili ambapo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam utakuwa shuhuda wa mechi kati ya Simba na Rhino Rangers kutoka Tabora wakati maafande wa JKT Ruvu na Mgambo Shooting watapambana Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam. Wakati huo huo, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka nchini, TFF amesema viwanja vyote ambavyo tayari vimefungwa mfumo wa elektroniki vitatumia tiketi za elektroniki isipokuwa ywanja wa Taifa, Dar es Salaam ambao wenyewe utachelewa kidogo ili kuangalia mfumo huo unavyofanya kazi katika viwanja vingine.


No comments:

Post a Comment