Friday, January 24, 2014

SUPER EAGLES KUWEKA KAMBI HOUSTON, TEXAS KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA.

MABINGWA wa Afrika, timu ya taifa ya Nigeria maarufu kama Super Eagles wanatarajiwa kuweka kambi yao jijini Houston, Texas, Marekani kwa ajili ya kujiwinda na michuano ya Kombe la Dunia litakalifanyika baadae mwaka huu nchini Brazil. Kocha wa Nigeria Stephen Keshi alikuwa amependekeza kikosi chake kuweka kambi yao ya mazoezi kati ya Miami au Houston lakini Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Soka nchini humo, Chris Green amesema wameamua kuchagua mji huo. Green amesema wamechagua mji huo kwasababu wanataka kufanya vyema katika michuano hiyo ambayo wanashiriki kwa mara ya tano hivyo wanapaswa kujiandaa vyema. Nigeria ambao wanatarajia kuanza kambi yao rasmi Mei 25 mwaka huu, wamefanikiwa kutinga hatua ya timu 16 bora katika michuano hiyo mara mbili mwaka 1994 na 1998. Green pia amesema timu hiyo imepanga kucheza mechi nne za kirafiki kabla ya mchezo wao wa kwanza wa Kombe la Dunia dhidi ya Iran utakaochezwa Juni 16.

No comments:

Post a Comment