Friday, January 24, 2014

HATMA YA KESI YA UZINZI YA KINA RIBERY NA BENZEMA KUJULIKANA ALHAMISI IJAYO.

WASHAMBULIAJI nyota wa kimataifa wa Ufaransa, Franck Ribery na Karim Benzema watarajia kujua hatma yao kama wameshinda kesi yao ya kumnunua mwanamke anayejiuza aliyekuwa chini umri Alhamisi ijayo baada ya mahakama ya jiji la Paris kuahirisha kesi hiyo kwa maamuzi zaidi. Mwendesha mashitaka Jean-ulien Xavier-Rolai aliomba wanasoka hao kuachiwa kutokana na kesi hiyo inayowakabili. Xavier-Rolai amesema ni suala lisilowezekana kupatikana kwa ushahidi kwamba Ribery alikuwa akijua mwanamke huyo aitwaye Zahia Dehar ambaye hivi sasa amekuwa mwanamitindo kuwa alikuwa chini ya umri wa miaka 18 kabla ya kuongeza kuwa Benzema pia anapaswa kuachiwa. Wachezaji hao ambao hawakuwepo mahakani wakati wa usikilizwaji wa kesi hiyo uliochukua siku nne wanatuhumiwa kwa kulipia huduma ya kingono kwa nyakati tofauti kwa Dehar wakati alipokuwa na miaka 16 na 17. Ribery alikiri kilipia huduma hiyo lakini alidai kuwa hakuwa akijua umri halisi wa Dehar wakati Benzema yeye alikana shitaka hilo na kudai hakuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamitindo huyo. Kulipia huduma ya kingono sio kosa nchini Ufaransa lakini kama anayejiuza akiwa chini ya umri ni kosa.

No comments:

Post a Comment