Sunday, January 26, 2014

RAMSEY NDIO MCHEZAJI KATIKA LIGI KUU UINGEREZA - VIEIRA.

NGULI wa zamani wa soka wa Ufaransa, Patrick Vieira anaamini kuwa kiungo wa Arsenal Aaron Ramsey ndio mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 amefunga mabao 13 katika mechi 27 alizocheza na kukisaidia kikosi cha Arsenal kinachonolewa na Arsene Wenger kukaa kileleni mwa msimamo wa ligi hiyo. Ramsey haakuwemo katika kikosi cha Arsenal toka kipindi cha Boxing Day mwaka jana kutokana na maumivu ya msuli lakini Vieira amesema nyota huyo wa kimataifa wa Wales amekuwa sehemu muhimu ya timu hiyo katika kampeni zao msimu huu. Akihojiwa Vieira amesema toka kuanza kwa msimu Ramsey amekuwa katika kiwango kizuri kwasababu ya mabao aliyofunga akitokea katikati lakini pia mabao kadhaa aliyotengenezea wenzake. Vieira ambaye kwasasa na mwalimu wa timu za vijana za Manchester City, pia alimpongeza Wenger kwa kuwapa nafasi chipukizi na kuamini kuwa wanaweza.

No comments:

Post a Comment