Thursday, January 30, 2014

SAMMER AMTAKA MANDZUKIZ KUPANDISHA KIWANGO CHAKE ILI AWEZE KUPATA NAMBA.

MKURUGENZI wa michezo wa klabu ya Bayern Munich, Matthias Sammer amemtaka Mario Mandzukic kuwa katika kiwango chake cha juu kwa msimu mzima uliobakia. Nyota huyo wa kimataifa wa Croatia aliachwa katika kikkosi cha timu hiyo ambacho kilishinda mabao 2-0 dhidi ya Borussia Monchengladbach na kuzua tetesi juu ya mustakabali wake siku zijazo haswa ukizingatia ujio wa Robert Lewandowski kiangazi. Hata hivyo, Sammer bado anaamini kuwa nyota huyo mwenye umri wa miaka 27 bado anaweza kuwa sehemu ya kikosi cha Bayern lakini anatakiwa kucheza kwa kiwango chake cha juu. Sammer amesema Mandzukic bado ni mchezaji muhimu kwao lakini kama akifanya kila analoweza kuhakikisha anarudi katika kiwango chake. Nyota huyo amecheza mechi 17 za Bundesliga msimu huu na kufunga mabao 10.

No comments:

Post a Comment