Thursday, January 30, 2014

CHAN 2014 FINAL: GHANA KUKWAANA NA LIBYA.

TIMU ya taifa ya Ghana, Black Stars imewashangaza mabingwa wa soka wa Afrika timu ya taifa ya Nigeria kwa kuwang’oa kwa changamoto ya mikwaju ya penati katika hatua ya nusu fainali ya michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani, CHAN jana usiku. Katika mchezo huo uliochezwa katika Uwanja wa Free State ulimalizika kwa sare ya bila ya kufungana mpaka katika muda wa nyongeza huku Ghana wakiwa pungufu ya mchezaji mmoja na kupelekea kupigiana mikwaju ya penati ambapo Ghana iliibua kwa ushindi wa matuta 4-1. Ghana sasa itachuana na Libya kaika mchezo wa fainali utakaochezwa Jumamosi jijini Cape Town ambapo hiyo itakuwa fainali yao ya pili katika michuano hiyo baada ya kupoteza kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC mwaka 2009. Libya wao walitinga haua hiyo baada ya wao pia kuindosha Zimbabwe kwa changamoto ya mikwaju ya penati 5-4 katika mchezo uliofanyika huko Bloemfontein.

No comments:

Post a Comment