Thursday, January 30, 2014

VETTEL ASONONESHWA NA HALI YA SCHUMACHER.

BINGWA wa mashindano ya langalanga, Sebastian Vettel ameonyesha wasiwasi wake juu ya hali ya dereva nyota wa zamani wa mashindano Mjerumani mwenzake Michael Schumacher kutokana na majeraha ya kichwa aliyopata. Schumacher ambaye ni bingwa mara saba wa mashindano hayo amewekwa katika dozi ya usingizi toka alipogonga kichwa chake katika jiwe wakati akiteleza katika barafu mwezi uliopita. Vettel ameelezea masikitiko yake kuhusiana na hali ya nyota huyo na kudai hawajui atakuwa na hali gani pindi atakapoamka kutoka katika dozi ya usingizi aliyopewa. Vettel amesema ni jambo gumu hususani kwa familia na marafiki zake wa karibu kutokujua kitakachotokea lakini wanamuombea kila siku aamke akiwa katika hali yake ya kawaida.

No comments:

Post a Comment