Monday, January 20, 2014

VIDIC AKIRI KUWA MAN UNITED MBIO ZA UBINGWA NDIO BASI TENA.

BEKI mahiri wa klabu ya Manchester United, Nemanja Vidic amekiri kuwa timu hiyo tayari imetoka katika mbio za ubingwa za ubingwa wa Ligi Kuu baada ya kukubali kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa Chelsea. Kipigo hicho cha United katika Uwanja wa Stamford Bridge kinakuwa cha saba msimu huu na kuwaacha wakiwa nyuma ya vinara wa ligi Arsenal kwa alama 14. Akihojiwa mara baada ya mchezo huo Vidic alikiri kuwa kwasasa wako mbali sana na wanatakiwa kuhamishia nguvu zao katika kutafuta nafasi ya tatu au ya nne kwenye msimamo ili waweze kupata nafasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya. Beki aliongeza kuwa sio jambo rahisi kushindana kujua kuwa wameshindwa kutetea taji lao katika kipindi hiki lakini hawana jinsi kwani bado kuna mashindano mengine ya kushindania kama Kombe la Ligi na Ligi ya Mabingwa.

No comments:

Post a Comment