Monday, January 20, 2014

ARSENAL YAMNYATIA VUCINIC WA JUVENTUS.

KLABU ya Arsenal inatarajia kuanza mazungumzo na wakala wa mshambuliaji wa Juventus Mirko Vucinic leo ikiwa ni mipango ya kocha Arsene Wenger kujaribu kuimarisha safu yake ya ushambuliaji. Wenger anataka kumchukua nyota huyo mwenye umri wa miaka 30 kwa mkpo wa miezi mitano lakini Juventus wanataka kumuuza kabisa ili watumie fedha hizo kuimarisha sehemu nyingine katika kikosi chao. Wakala wa mchezahuyo wa kimataifa wa Montenegro, Alessandro Lucci anatarajiwa kwenda jijini London kuzungumza na Arsenal katika siku hizo chache za mwisho kabla ya kufungwa kwa dirisha dogo la usajili. Hata hivyo Arsenal wanaonekana hawana haraka kuhusiana na uhamisho huo ambapo Wenger yuko tayari kusubiria mpaka masaa ya mwishoni kabla ya dirisha hilo kufungwa. Timu hiyo kwasasa imebakiwa na mechi mbili pekee kwa mwezi huu, ambapo wanakabiliwa na mchezo wa Kombe la FA dhidi ya Coventry City na mwingine wa Ligi Kuu dhidi ya Southampton.

No comments:

Post a Comment