Wednesday, February 19, 2014

AL AHLY KUIVUTIA KASI YANGA.

WAPINZANI wa timu ya Yanga katika michuano ya Klabu Bingwa ya Afrika, Al Ahly ya Misri watakabiliwa na kibarua kigumu kesho wakati watakapokuwa wenyeji wa timu ya CS Sfaxien ya Tunisia katika mchezo wa kugombea taji la Super Cup utakaofanyika jijini Cairo. Al Ahly itabidi wasahau matokeo mabovu ambayo wamekuwa wakipata katika mechi za ligi ya nyumbani msimu huu kama wanataka kuweka rekodi ya kunyakuwa taji la Super Cup kwa mara ya sita. Mechi hiyo ambayo huwakutanisha mabingwa wa Ligi ya Mabingwa msimu uliopita ambao ni Al Ahly na mabingwa wa Kombe la Shirikisho ambao ni Sfaxien unatarajiwa kupigwa katika Uwanja wa Taifa wan chi hiyo uliopo jijini Cairo ambao una uwezo wa kubeba mashabiki 75,000. Kocha wa Al Ahly Mohamed Youssef amesema anaamini mechi hiyo ni muhimu kwao kwani itawasaidia wachezaji wake kuongeza kujiaminina kusahau matokeo mabovu yaliyowaandama katika wiki za karibuni. Yanga tayari imeshatuma shushu wake katika mchezo huo ambaye ni kocha msaidizi Charles Boniface Mkwasa kwa ajili ya kuwapeleleza wapinzani wao hao kabla ya mechi yao itakayochezwa Februari 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment