Thursday, February 20, 2014

ROBBEN ALIZIDISHA CHUMVI - WENGER.

KOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger amemtuhumu Arjen Robben kwa kujirusha na kumponza kipa wa Wojciech Szczesny kutolewa nje kwa kadi nyekundu ambayo ilipelekea timu hiyo kulala kwa mabao 2-0 dhidi ya Bayern Munich jana. Mbali na kumlalamikia Robben, Wenger pia aliwalalamikia wachezaji wengine wa Bayern kwa kumtumia vibaya mwamuzi aliyechezesha mchezo huo Nicola Rizzoli. Wenger amesema hakuna shaka kwamba kipa wake alimgusa Robben lakini mchezaji huyo alizidisha chumvi kwa kujirusha zaidi hivyo kuharibu mchezo baada ya kadi nyekundu kutolea. Katika mchezo huo mabao ya Bayern yote yalipatikana katika kipindi cha pili kupitia kwa Toni Kroos na Thomas Muller baada ya timu zote kukosa penati katika kipindi cha kwanza ambapo Mesut Ozil alikosa penati kwa upande wa Arsenal huku David Alaba akikosa kwa upande wa Bayern. Kuna uwezekano kipa wa Arsenal akaadhibiwa zaidi na Shirikisho la Soka barani Ulaya, UEFA kwa kuonyesha ishara mbaya jukwaani wakati akitoka baada ya kupewa kadi nyekundu.

No comments:

Post a Comment