Thursday, February 20, 2014

NEYMAR AMTETEA BABA YAKE.

MSHAMBULIAJI nyota wa klabu ya Barcelona ameonyesha kukasirishwa kwake na rais wa zamani na sasa wa klabu ya Santos huku akimkingia kifua baba yake juu ya sakata la uhamisho wake kwenda Camp Nou. Nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 aliondoka nchini Brazil kwa ada rasmi ya euro milioni 57 ingawa mwezi uliopita Barcelona Barcelona ilitoa vielelezo vilivyoonyesha kuwa nyota huyo alisajiliwa kwa euro milioni 86.2. Rais wa sasa wa Santos Odilio Rodrigues ameishambulia kampuni ya baba yake Neymar kwa kulipwa bonasi ya kitita cha euro milioni 40 kama sehemu ya uhamisho ambapo klabu hiyo imechukua hatua za kisheria ili kuonya nyaraka zilizotumika katika makubaliano kati ya Barcelona na baba wa nyota huyo. Rais wa zamani wa Santos, Luis Alvaro de Oliveira Ribeiro pia alimshambulia baba yake Neymar akidai kuwa ni haki kabisa kupelekwa mahakamani. Neymar amesema amekaa kimya kwa kipindi kirefu lakini ameshindwa kwa jinsi watu aliokuwa akiwaheshimu wanavyomnyanyapaa baba yake. Nyota huyo aliendelea kusema kuwa haoni kosa alilofanya baba yake mpaka ashambuliwe hivyo kwani hata kama aliipata hela hiyo wanayosema hakuipata akiwa amekaa bali aliifanyia kazi kwa kipindi kirefu.

No comments:

Post a Comment