Thursday, February 20, 2014

STYLE YA UFUNDISHAJI WA MOYES NDIO INAYOMSHINDA VAN PERSIE - VAN GAAL.

KOCHA wa timu ya taifa ya Uholanzi, Louis van Gaal amedai kuwa mshambuliaji nyota wa klabu ya Manchester United anapata wakati mgumu kuzoea aina ya soka inayofundishwa na kocha David Moyes. Kuna taarifa kuwa Van Persie alikwaruzana na Moyes kutokana na aina ya mazoezi anayotoa msimu huu huku Shirikisho la Soka la Uholanzi likiwasiliana na United kuhusu majeruhi yanayomuandama nyota huyo kuelekea katika michuano ya Kombe la Dunia. Van Gaal anaamni kuwa mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal atakuwa fiti kwa Kombe la Dunia kwasababu mechi za timu ya taifa ni rahisi ukilinganisha na za United. Kocha huyo aliendelea kudai kuwa ana uhakika nyota huyo atang’aa akija katika timu ya taifa kama alivyofanya katika mechi zao za kufuzu kwasababu ni mahala ambapo anaweza kucheza kama alivyozoea kulinganisha na klabu yake.

No comments:

Post a Comment