Tuesday, February 4, 2014

KINNEAR WA NEWCASTLE AJIUZULU WADHIFA WAKE.

MKURUGENZI wa michezo wa klabu ya Newcastle United Joe Kinnear amejiuzulu wadhifa wake huo baada ya kuutumikia kwa kipindi cha nane. Kinnear mwenye umri wa miaka 67 alikuwa ndio bosi wa kocha Alan Pardew kwenye masuala ya utawala huku akitoa kwa mmiliki kuhusiana na masuala yote ya timu hiyo. Newcastle ilishindwa kusajili mchezaji yoyote wakati timu ikiwa chini ya Kinnear na Pardew amekataa kumuunga mkono kufuatia kipigo cha maba 3-0 walichopata kutoka kwa Sunderland Jumamosi iliyopita. Akihojiwa Pardew amesema kama angepewa nafasi ya kusajili pengine mambo yangekuwa tofauti lakini hakuwa na mamlaka hayo. Baada ya Newcastle kumuuza Yohan Cabaye kwenda Paris Saint-Germain kwa paundi milioni 19, timu hiyo ilishindwa kutafuta mbadala wake katika siku mbili za usajili wa dirisha dogo zilziobakia.

No comments:

Post a Comment