Sunday, February 2, 2014

LIBYA MABINGWA WAPYA CHANA.

TIMU ya taifa ya Libya wametawadhwa mabingwa wapya wa michuano ya Mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani, CHAN baada ya kuifunga Ghana kwa changamoto ya mikwaju ya penati katika mchezo wa fainali uliochezwa katika Uwanja wa Cape Town nchini Afrika Kusini. Libya walinyakuwa taji lao hilo la kwanza la kihistoria kwa kuigaragaza Ghana kwa penati 4-3 baada ya mchezo huo kumalizika bila ya kufungana mpaka katika muda wa nyongeza. Hiyo inakuwa mechi ya tatu kwa Libya kushinda kwa changamoto ya mikwaju ya penati baada ya kuziengua Gabon na Zimbabwe katika hatua ya robo fainali na nusu fainali. Kwa wa mechi ya kutafuta mshindi wa tatu Nigeria walifanikiwa kuibuka kidedea baada ya kuifunga Zimbabwe kwa bao 1-0.


No comments:

Post a Comment