Sunday, February 2, 2014

PAMOJA NA KUANDAMWA NA SARE SEEDORF ADAI MILAN INAIMARIKA.

MENEJA wa klabu ya AC Milan, Clerence Seedorf amedai kuwa klabu hiyo inaendelea kuimarika pamoja na kupata sare ya kufungana mabao 1-1 na Torino katika mchezo wa Serie A uliofanyika jana. Katika mchezo huo uliofanyika katika Uwanja wa San Siro wageni Torino ndio walioanza kupata bao kipindi cha kwanza kupitia kwa Ciro Immobile lakini wenyeji walirudisha bao hilo katika kipindi cha pili kupitia kwa Adil Rami. Sare hiyo inaonekana kumfurahisha Seedorf ambaye anadai kuwa wachezaji wake wameanza kuzoea mfumo anaofundisha. Seedorf amesema ni jambo jema kuona kikosi chake kikianza kuelewana taratibu na kudai kuwa ni dalili nzuri za kufanya vyema huko mbele. Sare hiyo imeiacha Milan katika nafasi ya tisa ya Serie A, wakiwa wanajikongoja toka alipotimuliwa kocha Massimiliano Allegri Januari mwaka huu.

No comments:

Post a Comment